Monday, December 31, 2012

MAMBO YA DIGITAL

eti nasikia kwenu mko digital kwa saaana mpaka mkiwa mnasafiri..mizigo na nmabegi yenu mnabeba kwenye flash disk......... happy digital 2O13

FESIBUKU

MAMBO YA MAHARI

Jamaa kaenda kuoa akaambiwa mahari million 5, akashangaa!!! 

Khaaaa! Million 5 wakati hapo kwa jirani nimeambiwa laki 2 tu tena mwanamke mwenyewe ana mimba kabisa tayari! 

Acheni masikhara! Ongeeni bei ya kueleweka.

Saturday, December 29, 2012

NOMA YAKE BANGIII...

Siku moja nyani alikuwa kakaa kijiweni anavuta bangi,mjusi{Lizard} akaja akampa ''Hi." akamjoin na kumuomba puff.

Nyani akamuonya kuwa ile bangi ni kali,ni kipisi cha kutoka Ukunda.Mjuzi akapokea wakaanza kuvuta kwa raha zao,mjusi akawa hoi kwa stimu akamwambia nyani,"Duh,nasikia koo langu limekauka acha niende mtoni nikanywe maji."

Mjusi kufika mtoni kwa kuwa alikuwa na stimu nyingi akatumbukia mtoni.

Mamba aliyekuwa pembeni akawahi kumuokoa na kumtoa nje ya maji.

Mamba akamuuliza,"Inakuaje bro,mbona kutumbukia kwenye maji kizembe vile!!"


Mjusi akajibu,"Nilikuwa na Nyani tunavuta bangi nikasikia kui ya ajabu,nikajikuta kwenye maji bila kujua!"


Mamba akasema,"Wacha niende huko kwa nyani nikamuone."

Mamba kufika akamkuta nyani ndo anamaliza kile kipisi hata macho taabu kufungua.Mamba akamuita,"Oya!!"

Nyani akafungua macho kumuona mamba akashtuka,


"Duh! Mshikaji,kwani umekunywa maji yote mtoni...mbona umerudi mkubwa hivyo!!"

UMEWEZAJE KUWA TAJIRI.....

A young man asked an old rich man how he made his money.

The old guy fingered his worsted wool vest and said, 

"Well son, it was 1932. The depth of the Great Depression. I was down to my last nickel. I invested that nickel in an apple. I spent the entire day polishing that apple and, at the end of the day, I sold the apple for ten cents.

The next morning, I invested those ten cents in two apples. I spent the entire day polishing them and sold them for 20 cents. I continued this system of polishing and selling, each time reinvesting my profits into buying more apples."

"Wow!" said the young man, "and that's how you accumulated your fortune?"

"Nah", said the old man, 

"my wife's father died and left us two million dollars."

Thursday, December 20, 2012

UKIWA JIKONI HISIKII KITU...

Bosi mmoja alikuwa na mazoea ya kununua wine anakunywa kidogo anaiacha juu ya kabati kisha anaenda kazini...lakini kila siku houseboy wake alieitwa Bakari alikuwa anakunywa kidogo alafu anaweka maji ili bosi asijue imepungua.

Bosi alihisi hali hii coz ilikuwa akiinywa tena baadae anakuta imebadilika ladha,siku moja akamuekea mtego kwa kununua wine ambayo ikiwekwa maji inabadili rangi na kuwa kama maziwa.

Kama kawaida bosi akanywa wine kidogo akaenda kazini,houseboy nae akaenda kama kawaida yake akanywa kidogo alafu akaweka maji...ghafla ikabilika rangi na kuwa kama maziwa...houseboy akachanganyikiwa akaenda kujificha jikoni.

Bosi aliporudi akakuta wine imebadilika rangi,akaanza kufoka,akamuita mke wake karibu na kumwambia leo tumeshika mwizi.

Bosi:"Bakari...wee Bakari!"
Bakari:"Yes boss."
Bosi:"kwanini umekunywa wine wangu na ukaweka maji?
Bakari:[Kimya]
Bosi:"Kwanini umekunywa wine yangu?"
Bakari:[Kimya]

Bosi akapandwa na hasira akamfuata bakari jikoni huku mkewe akiwa nyuma.
Bosi:"Nimekuita umeitika,lakini swali langu hujibu kwanini?

Bakari:"Bosi ukiwa huku jikoni hausikii kitu chochote isipokua jina lako tu,kama huamini baki humu ndani ujionee.

Bakari akatoka nje na mke wa bosi na kumwacha bosi ndani.
Bakari:"Boss."
Bosi:"Yes Bakari."
Bakari:"Nani hupenda kuingia chumba cha housegal wakati madam boss yuko kazini?"
Boss:[Kimya]
Bakari:"Nani hulala na housegal wakati madam boss amesafiri?"
Boss:[Kimya]

Bosi akafungua mlango wa jikoni,akatoka na kusema:"Walai maajabu ukiwa humu ndani huskii chochote isipokuwa jina lako tu!"

Mke wa bosi akaja juu:"Pumbavu! Waongo wakubwa nyie...nini kinaendelea hapa enh??"

Bakari:"Ukweli mama ukiwa ndani unasikia jina lako pekee....kama unabishana ingia utaamini!"

Mke wa bosi akaingia jikoni na kumwacha mume wake na bakari nje.
Bakari:"Madam?"
Mke:"Yes Bakari?"
Bakari:"Sema ukweli nani baba yake mtoto kati ya mimi na bosi?"
Mke:[Kimya]
Bakari:"Eeh..tuambie nani aliyekupa hio mimba?"
Mke:[Kimya]

Akafungua mlango akatoka:"Aaah...ni kweli,humu ndani kunahitaji maombi,yaani ukiwa ndani unasikia jina lako pekee!"

Saturday, December 15, 2012

MAMBO YA KAMARI

ENEO MARIDHAWA

WENGINE HAMNAZO....

Jamaa alikuwa amechoka na kaz akaamua kufanya kituko ili apewe likizo au aambiwe akapumzike nyumbani.


Asubuhi ilipofika jamaa akaenda akajining‘iniza kwenye dali kama taa.



Bosi alipofika akashangaa na kuuliza 


‘unafanya nini huko juu??‘

Jamaa:mm ni taa namulika ofisi 


Bosi:naona kazi inakupa stress. nenda nyumbani ukapumzike.

Jamaa akashuka na kuanza ondoka na rafiki 

yake pale ofisini naye akainuka akamfuata nyuma.



Bosi akashangaa na kumuuliza rafiki 





‘na ww unaenda wapi??‘



Rafiki:sasa nitafanyaje kazi kwenye giza boss??



Tuesday, December 11, 2012

KASUKU MATATA

Mwanadada mmoja mrembo alienda mjini kufanya shopping,akapita mahali flani akaona muuzaji mmoja anauza kasuku elfu 25....akaamua kuulizia:

Dem:"Mambo."

Muuzaji:"Poa sista...nikusaidie nini?"


Dem:"Nilikuwa naulizia tuh...inaonekana huyu kasuku wako ni special maana unamuuza kwa bei ghali!"

Muuzaji:"Huyu kasuku huongea ndio maana namuuza kwa hio bei."

Yule dem akaamua kumjaribu pale pale...akamuuliza kasuku, "Mmmh..hebu niambie leo nakaaje?...mi najiona nimetoklezea!"

Kasuku akajibu:"Unaonekana kama MALAYA..."

Dem akakasirika na kusema,"Siwezi kumnunua kasuku huyu maana ni mshenzi ana tabia mbaya na za kipumbavu!!"

Muuzaji akamwambia yule dada asubiri kiasi...akamchukua kasuku na kuenda nae nyuma ya duka,akamzamisha ndani ya beseni lililojaa maji kwa dakika kadhaa...kisha akamtoa na kumwambia,"Pumbavu ukirudia kuongea ushenzi mbele ya wateja kama yule dada nitakuzamisha tena na safari hio hadi ufe...mshenzi wewee!!"

Aliporudi akamkuta yule mwanadada bado yupo akamwambia,"Dada samahani kwa tatizo hilo...naomba umuulize tena kasuku swali lolote."

Dem akauliza:"Nikirudi nyumbani kwangu na mwanamume mmoja utafikiriaje?"

Kasuku:"Kwa kweli nitafikiria huyo ni MUME WAKO."

Dem:"Nikirudi na wanaume wawili?"

Kasuku:"Hapo itakuwa MUME WAKO na KAKA YAKO."

Dem:"Je nikirudi nyumbani na wanaume watatu?"

Kasuku:"Hao watakuwa MUME WAKO,KAKA YAKE MUME WAKO na KAKA YAKO."

Dem:"Vipi je nikirudi nyumbani na wanaume wanne?"

Kasuku:"Aarggh!..Kudadeki!!! Lete hilo beseni la maji....nilishakwambia huyu dada ni MALAYA...!!!"

Saturday, December 8, 2012

BANGI HAIONGOPI.....

Mzee mmoja alikuwa anasumbua vijana waliokuwa wanavuta bangi nyuma ya nyumba yake na kuwatishia atawaitia polisi.

Siku moja wakati wale wavutaji bangi wanavuta vitu vyao wakapanga jinsi ya kumkomesha yule mzee ili asiwasumbue tena.

Mmoja wao akatoa wazo la kuisukuma nyumba ya yule mzee ili isonge mbali na eneo wanalovutia bangi...wote wakaunga mkono wazo hilo.


Wakavua mashati yao wakaanza kusukuma nyumba,wakati wanaisukuma yule mzee akapita akachukua mashati yao na kuyasongeza mbali bila wale wavuta bangi kumuona.

Walipochoka kusukuma,wakageuka kuchukua mashati yao walipo ona yako mbali na ile nyumba....wakaanza kupongezana,"Lo! Leo tumefanya kazi kweli...kesho tutaendelea kuisukuma mpaka itoke mtaani kwetu!!"



VITUKO MAOFISINI

Jamaa mgeni kabisa kaajiriwa kwenye kampuni-akapewa supervisor mwanamke.

Supervisor: mheshimiwa, unaitwa nani?


Jamaa: Naitwa John...

Supervisor: John nani? Unajua jambo ambalo nimegundua ni kua watu wakiaanza kuitana kwa majina ya kwanza, mnazoeana na kazi haitofanyika. Mie si rafiki yako, mimi ni supervisor wako. Kwa hivyo nipe jina lako la pili upesi ndio nitakalokuita nayo!

Jamaa: naitwa John Mmewangu.

Supervisor: haya bwana John, endelea na kazi..



MAPENZI YA FESIBUKU....KUOMBA MSAMAHA

BOY: Baibe, i know i did u wrong but i just ask 4 ua forgiveness....

GAL:[message seen] 3minutes ago.


BOY: Hunnie, pliz just forgive me... am a human being and am not perfect neither are you...

GAL:[message seen] 2minutes ago.

BOY: U remember insulting me the other day? Did i not forgive u swits?

GAL:[message seen] 2minutes ago.

BOY: Hunnie pliz, dont do this to me ... i love u and i dont wanna luz u....

GAL:[message seen] 3minutes ago.

BOY: Listen baibe, right now as i am, i have just received my salary and i have put aside ksh.35,000 just to go out with u, do some shopping, go to a big hotel and just have a nice time to make it up to you.... are u gonna join me hun?

GAL: Woow! Thats awesome hunnie, where should i find u baibe? i cant wait to make up with u my love

BOY:[message seen]
just a minute ago.

GAL: Darling are u still there?

BOY:[message seen]
2minutes ago.

GAL:Oooh dear! pliz dont do this to me hun... i know u are still there......

BOY:[message seen] 2minutes ago... logging out.






Monday, December 3, 2012

TUNAENDA ULAYA

Jamaa alimkuta mwanamke mmoja pale Ferry analia, akamuuliza shida, yule mdada akasema maisha yamemshinda anaona heri ajiue.

Jamaa akamwambia kuwa yeye ni baharia kwa hiyo akikubali atamuweka kwenye boksi 

kisha atamficha kwenye meli yake na wataweza kusafiri mpaka Ulaya wakifika huko atamuoa.....



Bibie akaona heri hilo akaingia kwenye boksi jamaa akambeba na kweli mdada akajikuta yuko kwenye stoo moja wapo katika meli...



Jamaa akawa anamletea chakula kila siku na mara nyingine yeye mwenyewe analala huko kwenye hako kastoo akikonga nyoyo na yule mwanamke na kujivinjari naye huku akizidi mhakikishia mdada kuwa wanakaribia visiwa vya Komoro then wataingia Ulaya!!!! 





Kisha akatoka na kuendelea na shughuli zake...


Zikapita wiki nne ndipo yule mdada akagundulika na nahodha wa chombo hicho, alipoulizwa akalazimika kueleza kila kitu, na kuwa anamuomba nahodha asimtupe baharini bali amlinde mpaka watakapofika Ulaya....


Nahodha akamwambia mdada,



"Wala usipate taabu, ila jamaa yako kakudanganya hii si meli ya kwenda Ulaya ni pantoni ya kwenda Kigamboni, tukifika huko we shuka.... Pole kwa kushinda humu siku zote hizo!!!"'



Sunday, December 2, 2012

NANI MUUAJI??

SHULE YA MSINGI JANJAJANJA...

Ticha: Ni nani aliyemuua Chifu Mkwawa?

Dent 1: Sio mimi!

Dent 2: Walla sihusiki.!

Dent 3: Kwanza mimi jana sikuja shule.!

Ticha alipoona kuwa wanafunzi wote ni majuha, akaamua kumuita Mkuu wa shule. 

Mkuu akawauliza swali lile lile,

majibnu ya wanafunzi yakawa vile vile, Ndipo Mkuu alipomuita Mwalimu pembeni na kumnong'oneza.

"LAKINI UNA UHAKIKA MUUAJI YUPO DARASA HILI?"