Friday, April 12, 2013

HAUKO SIRIASI


Simu ya binti inaita ngriiiiiiiiiii ngriiiiiiiiiii. Binti anapokea. Jamaa upande wa pili akaanza:
Jamaa: Haloo mpenzi, vipi hali yako?

Binti: Kichwa kinanigonga si mchezo, sijui ni maleria au ni kichwa tu! Naumwa sana. Uko wapi swirii?

Jamaa: Niko town my dear. Natamani nije kukuona baadaye, nikuletee nini?

Binti: Wow! Mpenzi unanipenda sana. Niletee Chipsi Kuku, Ice Cream, Chocolate, na lile gauni na viatu ulivyoniambia, na vocha ya buku 10 please!

Jamaa: Nilikuwa najua unaumwa ila naona uongo umekuzidi.

Binti: Khaa, naumwa mwenzio! Tena sana. Kwani vipi we mwanaume?!

Jamaa: Na mbona hiyo list ya vitu umetaja hakuna hata Panadol?!

Binti: Jamani, ni kujisahau tu mpenzi wangu!

Jamaa: Hauko serious! Chapa mwendo.

No comments:

Post a Comment