Saturday, July 27, 2013

ZUZU TASLIMU

MSICHANA: Namchukia mvulana wangu.

ZUZU: Kwa nini?


MSICHANA: Yaani ni mtu wa bei rahisi sana, hawezi hata kuninunulia dinner. Hivi wanaume wote mpo hivyo?


ZUZU: Hapana. huyo yeye tu, sisi hatupo namna hiyo. Hata mimi sipo namna hiyo.


MSICHANA: Nakwenda kuachana nae leo hii hii.


ZUZU: Sawa. Ila utakapoachana nae, unaweza kuja kwangu, sina msichana halafu nakuhitaji sana.


MSICHANA: (Akasimama na kutaka kuondoka, ZUZU akamshika mkono)


ZUZU: Ndio unataka kuondoka? Unakwendawapi sasa?


MSICHANA: Nakwenda kuvunja uhusiano na yeye ili niwe nawe kwa uhuru.


ZUZU: Hapana. Huwezi kuondoka.


MSICHANA: Kwa nini?


ZUZU: Sasa ukiondoka nani atakayelipia hiki chakula tulichokula!


No comments:

Post a Comment