Tuesday, June 3, 2014

MUNGU ANASEMAJE??

MWALIMU Kasinzia darasani , DOGO kamfuata na kumwambia Teacher mbona umetupa zoezi tufanye alafu unasinzia ?? 

[MWALIMU:] ''hapana mimi sijalala !"

[DOGO]: ''kwani hapa ulikuwa unafanya nini mda huu ? mimi nimekuona umelala''

[MWALIMU:] ''nilikuwa naongea na MUNGU!''

KESHO YAKE

DOGO kasinzia Darasana wakati kipindi linaendelea. MWALIMU akamuamsha
"DOGO, Yani unathubutu kusinzia kwenye kipindi changu?"

[DOGO:] "Hapana mwalimu sijasinzia!"

[MWALIMU:] " Enhee Tuambie Basi ulikuwa unafanya nini ? maana darasa zima limekuona"

[DOGO: ] "nilikuwa naongea na MUNGU na mimi Pia "

MWALIMU Kwa Hasira huku akipiga kelele , " Enhe Hebu Tuambie MUNGU wako Amesemaje ???!?!" maana naona watu mnatafuta Viboko Asubuhi Asubuhi.

[DOGO:] "MUNGU Kasema Hakuongea na wewe Hapo Jana !"


No comments:

Post a Comment