Tuesday, June 3, 2014

STUPID

DOGO: Eti baba mtu stupid yuko je? 


DADDY: Hilo ni swali zuri sana, a very good kweshen kwa kweli I am praud of you,ni wazi kuwa kuna kila sababu ya kukiri kuwa elimu unayopata inaendana na mtizamo mzima wa big results now, you see mwanangu, mtu stupid ni yule ambaye akiulizwa just a simpo kweshen, yaani swali dogo sana basi huanza kulinyumbulisha na kuongeza mofimu na fonimu katika hilo swali, kuanza kutafuta, tena infact bila mantiki yoyote wala kufuata basis ya swali, na baada ya hapo kufanya mchanganuo usio na mashiko yoyote na hatimae kukam up na solushenz ambazo in prinsipo hazikuweko katika swali husika kiasi cha kwamba aliyeuliza swali anakuwa haelewi hata kitu, umeelewa 


DOGO: Hapana


No comments:

Post a Comment