Monday, March 18, 2013

ENDELEA KULIA

Nimemkuta rafiki yangu analia kama mtoto mdogo chumbani kwake;

MIMI: Oya mshkaji vipi tena nani kafa?


MSHKAJI: Yaani Gulo kaniuwa, hivihivi bila kosa kaniuwa


MIMI: Hebu tulia nambie ishu nzima


MSHKAJI: Si unajua nimekuwa namlipia Gulo ada toka sekondari mpaka sasa yuko chuo nikijua ndio niko peke yangu na nitamuoa?


MIMI: Ndio


MSHKAJI: Jana nikataka kuangalia kanisevu nini kwenye simu yake


MIMI: Ok


MSHKAJI: Si kanisevu eti Mchungaji Peter 12


MIMI: Sasa tatizo liko wapi


MSHKAJI: Nilipoangalia majina mengine sinimekuta kuna Pasta Hamfrey, Pasta Henry, Askof Kitime , na kuna Mchungaji Peter 1 mpaka mimi wa 12, wakati hata siku moja haendi kanisani wala maombi


MIMI: Dah endelea kulia mwanangu


No comments:

Post a Comment