Wednesday, November 19, 2014

GM

MKAKA: Mambo mrembo?

MDADA: Safi

MKAKA: Tafadhali naomba nizungumze machache na wewe

MDADA: We vipi kila mwanamke ukimuona unataka kuongea nae

MKAKA: Nisikilize kwanza, mi mtu mzima nina akili zangu siwezi kukusimamisha bila sababu

MDADA: Ok unasemaje?

MKAKA: Asante kwa kunipa muda, mimi ni GM hapo benki, ndugu zangu wamekuwa wakinilazimisha nioe nimekataa muda mrefu, nilipokuona tu roho imenisimama, nataka kukuoa basi

MDADA: Umesema GM wa Benki?

MKAKA: Ndio mrembo wangu nimekuwa GM hapo mwaka wa tatu sasa

MDADA: Wooow, hata mimi najiona muda wa kuolewa umefika, kuolewa na GM itanihakikishia maisha ya uhakika na mimi nitakutunza mume wangu, njoo nyumbani wakujue

MKAKA: Basi tufanye kesho, ili niombe ruksa kwa wakubwa waniruhusu kesho niwe off

MDADA: Kuomba ruksa kwa wakubwa? Mbona sikuelewei? We si ndio GM?

MKAKA: Ndio mimi GM yaani Gate Man sasa lazima niombe ruksa au nitapoteza kazi

MDADA: Mshenzi mkubwa unanipotezea muda wangu, najua naongea na mtu wa maana kumbe mfungua geti kwandraaa zako

No comments:

Post a Comment