Tuesday, January 29, 2013

MATEJA


Mateja fresh wawili walikuatana barabarani, mmoja akamshangaa mwenzie kumuona ana baiskeli nzuri kweli na kwa uteja wao hakuweza kupata jibu jamaa kaipata wapi?

Hivyo akamuuliza,

TEJA 1: duh! Mwana bonge ya baiskeli, umeipata wapi?? Sidhani kama umenunua lazima utakua umepora tu, ngoja wakudake?

TEJA 2: aah mwanangu mwenyeeewee, sijanunua, sijaiba wala nini yaani?

TEJA 1: (kwa mshangao) hee! Sasa umeipata wap??

TEJA 2: nilikua nakatiza kitaa cha beach, akaja mrembo mmoja wa ukweli anaeiendesha…. Akasimama kasha akanicheeki akaitupa baiskeli chini na kuvua nguo zoote.. akajilaza chini ananiambia.. "chukua chochote unachotaka.. hii ndo bahati yako zali la mentali".

TEJA 1: aah bora umechukua hiyo, maana kwa vyovyote nguo zake zisingekutosha





No comments:

Post a Comment