Friday, January 4, 2013

MIZINGUO YA DADA KIBOGA

MASANJA: niaje mrembo?

DA KIBOGA: we unaona aje? 

MASANJA: nacheki umeiva ile sirias yaani...

DA KIBOGA: sasa juu ya hiyo unatakaje?

MASANJA: mmmmh... mi nataka tu tuwe mabeshte....

DA KIBOGA: kwani sahizi tupo kama maadui?

MASANJA: hahaha... sio hivyo, yaani, i mean tuwe closer than before...

DA KIBOGA: kwani sahizi tuko opener than before?

MASANJA: hehehe.. dah... si maanishi hivyo, i mean, nataka tuwe tunatembeleana... si unajua

DA KIBOGA: ati tunatembeleana? sasa kama viatu yako vina uchafu, ukinitembelea utanichafulia nguo... na kwanza ulivyo mzito, ukinitembelea nitavunjika na nipelekwe hospitali?

MASANJA: ai wewe... simaanishi hivyo, namaanisha tuwe tunaonana every now and then....

DA KIBOGA: sawa basi... ntakuletea picha yangu na wewe uniletee yako na uwe unaangalia yangu na mimi ntakua naangalia yako ... sawa?

MASANJA: yaani mimi ndo unanichezea akili hivyo kama mtoto? ...

DA KIBOGA: nimeichezea aje? si unaniona hapa? kwani nimeingia kwa kichwa chako?

MASANJA: acha hata niende... naona hatusaidiani.

DA KIBOGA: ulikua unataka tusaidiane kwani uliskia mimi ni member wa red cross au UN?



No comments:

Post a Comment