Thursday, August 23, 2012

NDOTO ENDELEVU

Kuna jamaa mmoja alikuwa kila siku usiku akilala anaota NGEDERE na PANYA wanacheza mpira ikabidi siku moja aende hospital kumuona dokta alipofika hospital mazungumzo yakawa hivi:-

JAMAA: "Dokta mimi nimekuja ninasumbuliwa na ndoto kila siku usiku nikilala naota Ngedere na Panya wanacheza mpira utanisaidiaje?"


DOKTA: "Kwa hilo tatizo lako ulilosema inabidi nikupe hizi dawa ukifika nyumbani uzimeze, ukizimeza kuanzia leo hauto ota tena ndoto hizo sawa!"


JAMAA: "Sawa dokta ila itabidi nianze kuzimeza kesho kwakuwa leo ndio Fainali nataka nijue nani atashinda katika mechi ya leo"


- Dokta alibaki anashangaa!


No comments:

Post a Comment