Sunday, July 8, 2012

HATA UKO PIA??

Mchungaji flani baada ya kumaliza sala akawambia waumini wafumbe macho ili waombe.

Walipofumba macho wote mchungaji akaingiza mkono kwenye sanduku la sadaka na kuiba pesa....ile anatoa mkono akakutana uso kwa uso na mzee aliyekuwa anaingia kanisani.


Mchungaji akasema "Amebarikiwa mtu yule anayeshuhudia kwa macho yake na kubaki kimya..."

Mzee akamalizia "Kwa sababu atapata malipo yake baada ya ibada!"


No comments:

Post a Comment