Thursday, July 12, 2012

WATOTO WENGINE KIMEO


Watoto wengine kimeo

Joti karudi nyumbani siku hiyo akitokea shule huku akiruka ruka na kuimba na kucheza… baba yake, Mpoki, kumuona vile akashangaa, mbona leo dogo anarudi akiwa na furaha namna iyo na haiwi ivo siku zote?

Mpoki akamuuliza 

“eeeh mwanangu imekuaje leo umekua na furaha namna hiyo kuliko siku zote na hata sijawahi kukushuhudia ukiwa namna iyo??...vipi kuna nini mwanangu??”

Joti akajibu

“aisee baba, mwaka huu wala hautahangaika kuninunulia vitabu vipya, madaftari mapya na vingine kama hivo..kwa mwaka mzima”

Mpoki akafurahi akasema 

“ aaa aisee safi sana mwanangu, yani ndio mana nakupenda….."

(gafla akashtuka, akahoji)

“hebu ngoja kwanza…………………….. kwanini unasema sitanunua hivyo vyote umefanyaje mwanangu??”

Joti akajibu kwa kujiamini

“aaaah si nimerudia darasa lile lile baba...”

No comments:

Post a Comment