Tuesday, June 5, 2012

UKISIMAMISHWA NA TRAFFIKI

Ukisimamishwa Na Tirafiki Ukisema Haya Hawakuachi 

1. Ilikuwa na mimi niwe polisi sema tu niliamua kuendelea na shule!


2. Vipi hali ya biashara? Kijiwe kinasemaje? Naona neema zinakutiririkia tu!


3. Nimetoka kumcheki jamaa angu anafanya hapo Takukuru nikaona nigeuzie hapa hapa!


4. Naona mama Bhoke maji yanakaribia kukauka jikoni!


5. Jana si nilikutoa kiongozi? Leo hali mbaya!


6. Nna hakika nyumba ndogo huwa zinafanya watu wafanye vitu hawapendi kufanya makazini!


7. Ile gari ya nyuma yangu wapo Jeri Muro na Saidi Kubeneya.


8. Iko siku Jakaya atapita janksheni kwa janksheni!


9. Kiongozi naona unajazilizia mtaji!


10. Naona umetuuuuna unakula kwa urefu wa kamba yako!


11. Kazi nafanya Takukuru ila niko likizo kidogo!


12. Kakaaa naona unakazana kumalizia ile nyumba yako ya Bunju!


No comments:

Post a Comment