Wednesday, June 27, 2012

VIOJA BARABARANI..


Hii imetokea juzi ruti ya kutoka Sinza kuelekea Posta mishale ya saa 3 asubuhi.

Kulikua na daladala imekula nyomi kama kawaida asubuhi kwenda town watu wanajaa tangu mwanzo wa basi kwa hiyo njiani kunakua hakuna haja ya kupakia tena……

Madereva wengi huamua kuchepuka na kupita vichochorni watokee magomeni kasha washushe jangwani, faya waingia mjini mapema wanede na kugeuka fasta.

Juzi dereva mmoja akafanya hivyo ili apite kama tandale uku aibuke magomeni kisha aenda town… kwa bahati mbaya  Trafiki walikuwepo alikopita akasimamishwa..

TRAFIKI: nyie ndio tunawatafuta siku zoote

DEREVA: kwanini muheshimiwa

TRAFIKI: mnajifanya mna haraka humu duniani kuliko watu wote sio??

DEREVA: hapana muheshimiwa ila hii gari imekodishwa kwa ajili ya harusi.

(abiria kwa nyuma wanasikilizia kinachoendelea)

TRAFIKI: (Aking’aka) aaah unanifanya mi zumbukuku sio… yani ndio wajizidishia makosa sasa gari linawekwa ndani na we mwenyewe dereva unaenda ndani(selo).

Abiria kusikia ivo, mmoja kwa nyuma akaanzisha,

…dada huyoo anaolewa…. Dada huyoo anaolewa.. 

(abiria wote wakaanza kuitikia)

Mahariiiii..... ishatolewaaa...  Dada huyooo anaolewa….dada huyooooo anaolewa….!!!

(trafiki akaona apo ameshindwa akaruhusu gari liendeleee…)

1 comment: