Saturday, June 30, 2012

USIFICHE TATIZO LAKO KWA MWENZI WAKO


Hii ilimtokea jamaa mmoja ambaye alikua na mpenzi wake na wakaja kuoana. Kila mmoja kumbe alikua na tatizo lake na amekua akilionea aibu hivyo hakuna aliyethubutu kuliweka wazi kwa mwenzie kwaio walikua wanajaribu na wanafanya kila mbinu kulificha ili mwingine asigundue.

Jamaa tatizo lake kubwa ilikua ni Kwamba akivaa viatu tu pale anapovua miguu yake inatoa harufu balaa…. Kwaio dawa yake ilikua akirudi tu anavua viatu na alikua na soksi maalumu anavaa papo apo so inapunguza ile makitu au havui soksi kabisa.

Vile vile mkewe akikua na tatizo la kunuka mdomo ile mbaya hasa anapolala tu pindi akiamka, hata alale kwa muda mfupi harufu yake inakua balaa kwaio dawa yake ilikua akiamka tu hasemi neno wala kupiga muayo anawahi bafuni na kupiga mswaki kurekebisha mambo.

Siku moja, kama kawaida yake jamaa kapiga mtungi yuko nduki balaa (kalewa) akarudi nyumbani kwake mishale ya saa 6 usiku. Akaingia ndani na kupitiliza kulala mana tungi lilizidi hivyo alishindwa kufanya zoezi lake la soksi. Akakuta mkewe amelala naye akajilaza na kupiga mbonji.

Ilipofika saa 10 na nusu alfajiri jamaa akastuka na pombe kidogo imekata kujipekua akakuta soksi moja hakuna na kale kaharufu anakasikia akaona duh hili soo…. Uku pombe ikiwa kichwani akaanza kuitafuta pasipo mafanikio.. la mwisho akaona hana jinsi bora amuamshe mkewe amuulize soksi yake iko wap..

Akaanza kumuamsha mkewe…

“weee…. Amka aisee kuna kitu nakitafuta sikioni”

Wakati huo mkewe usingizi umemkolea na kama ujua kausingizi ka ule mda kanakua katamu ukiamshwa unaona kero… akataka aitike ila akakumbuka duh akiitika tu ile harufu ya mdomo itatoka na litakua soo kwaio akauchuna.

Jamaa akaamsha tena si wajua kelele za mlevi zinavyoboa?

“wee mwanamke si nakuamsha mimi wajifanya umelala??....amkaa aisee”

Mwanamke kwa hasira akageuka akasema

“aaaaaaah…..nini??” mbele ya uso wa jamaa

Duh jamaa akakutana na ile harufu live…akastuka!!

“wee mwanamke duh…yani umekula soksi yangu???
Tema nakwambia tema!!!!”

1 comment: